Thursday, August 12, 2010

WAZIRI WA ZAMANI AFIKISHWA MAHAKAMANI


Waziri wa mkongwe wa serikali ya awamu ya kwanza hadi ya nne na aliyekuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini, Joseph Mungai amefikishwa jana katika Mahakama ya Mkoa wa Iringa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma za kutoa rushwa wakati wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kesi yake iko kwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa, Mary Senape na kwamba anatuhumiwa kufanya kosa hilo Julai 8, mwaka huu katika Kata ya Ihalimba.

No comments:

Post a Comment