Tuesday, August 31, 2010

VYAMA VINNE HAVIJAZINDUA KAMPENI MPAKA SASA

Ndugu wadau, nitaendelea kuwaletea matukio mbalimbali ya uzinduzi rasmi wa kampeni ya vya vingine ambavyo hajazindua mpaka sasa. Vyama ambavyo havijazindua ni TLP, UPDP, NCCR-Mageuzi na APPT- Maendeleo.

Mgombea urais wa TLP ni Mutamwega Mugahywa, UPDP ni Fahmi Dovutwa, NCCR-Mageuzi ni Hashim Rungwe na mgombea urais wa APPT- Maendeleo ni Peter Mziray, lakini Mziray anadai chama chake kimezindua kampeni ingawa hakijaonekana kikifanya hivyo. Baadhi ya wagombea ubunge na udiwani wa vyama hivyo, wameanza kampeni.

Kumekuwepo malalamiko kwa waandishi wa habari kutoandika habari za vyama vingine vidogo. Baadhi ya watu wanadai waandishi wanaandika habari za vyama vitatu tu yaani za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chadema na za Chama cha Wananchi CUF. Mgombea urais wa APPT- Maendeleo, Mziray anasema waandishi wanaandika habari za vyama ambavyo vinaweza kulipa gharama za waandishi hao. Kwa upande wangu naahidi kufuatilia habari za vyama vingine.

CHADEMA YAZINDUA KAMPENI JANGWANI JIJINI DAR ES SALAAM



Dk Willibrod Slaa akiwatubia wanachama na mashabiki wa Chadema katika uzinduzi wa kampeni za katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam, juzi. Picha zote na Emmanuel Herman.

Wanachama na mashabiki wa Chadema wakimsikiliza mgombea urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho.


Kushoto ni Fred Mpendazoe, katikati John Shibuda na kulia, ni Bob Makani wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za Chadema kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam juzi.

USWAZI JIJINI DAR ES SALAAM





Hapa ni Manzese jijini Dar es Salaam

Monday, August 30, 2010

WANAHABARI MMEPOTEA KATIKA TAALUMA YA HABARI

Ndugu mwana mapambano mwenzangu , mwanahabari na mwanaharakati mwenzangu , naomba kutumia fursa hii katika blog yako kuweka wazi au bayana juu ya hoja hii ya taaluma ya habari na vyombo vya habari kukiuka maadili ya kitaaluma .

"Kumeanza pia kujitokeza mtindo wa baadhi ya vyombo vya habari kutoripoti kabisa habari za baadhi ya vyama na wagombea. Baraza linapenda kuwakumbusha wenye vyombo vya habari na wahariri wao kuwa kibali cha kuendesha gazeti au kituo cha radio au runinga ni mali ya umma.

Leseni za vyombo vya habari hutolewa ili umma upewe taarifa; hili ndilo lengo la kwanza. Faida ya kifedha au mapenzi ya kisiasa sio sababu kuu inayofanya leseni ya chombo cha habari itolewe. Kwa hiyo wahariri wajitahidi kufanya kazi yao kwa uadilifu, na wamiliki wa vyombo wasiwashinikize kuacha kutangaza au kuandika habari muhimu katika kipindi hiki."
Hayo si maneno yangu ni manenno ya katibu mtendaji Baraza la Habari Tanzania , aliyosema kwa lengo la kutoa onyo kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari .
Naweza kusema kama alijua kuwa wanataaluma ya habari pamoja na vyombo vya habari vimepotea katika taaluma hii , kama ilivyo ada waandishi na vyombo vyake wamekuwa vibaraka wa wagombea wa chama fulani katika kutangaza sera zake , kitendo cha televisheni ya Taifa (TBC) kukatisha hotuba ya mgombea kiti cha urais kupitia chama cha Chadema ni uvunjaji wa sheria na kukiuka haki ya msingi ya wananchi wa Tanzania katika upataji wa taarifa au habari .
Naaamini kabisa katika hali ya kawaida kituo kikubwa kama TBC na kinachoendeshwa kwa kodi za wananchi ni aibu kukatisha matangazo katikati ya hotuba kwa zaidi ya mara moja , ikumbukwe kuwa hii si mara ya kwanza dalili hizi au hali ilishajitokeza hata siku ile ya mgombea wa Chadema alipokuwa anaomba ufadhili .
Ni vyema tukakumbuka kuwa kutokuwepo kwa usawa katika vyombo vya habari ni dalili tosha za kusababisha uvunjaji wa amani ni vyema tukakumbuka juu ya mahuaji ya kimbali kule Rwanda na Burundi sekta ya habari ina nguvu kama sekta zingine za kitaifa , ifahamike kuwa watanzania kwa sasa wanajua haki zao zote na wanafaham nini kinaendele katika Taifa la Tanzania .

Ushauri wangu ni kuwa kwa vile TBC ni chombo cha kitaifa na kinawajibu wa kuwajibika kwa umma ni vyema Mtendaji Mkuu wa hicho chombo awaeleze umma juu ya swala hili kwani kuna hisia kali baina ya TBC na vyama vya upinzani katika kutokuwepo usawa wa kutoa taarifa na mbaya zaidi hii inaonekana wazi .




Mwandishi wa makala haya

ni Samwel Mtuwa

Anapatikana Minnesota ,

United State of America (USA)



Saturday, August 28, 2010

KESI YA KINA JERRY MURO YAAHIRISHWA


Washitakiwa wa kesi ya kuomba rushwa wakijadiliana jambo kwenye kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana,baada ya kesi yao kuahirishwa mahakamani hapo jana,kutoka kulia ni Edmund Kapama,Deogratias Mgasa na Jerry Muro.Picha na Michael Matemanga
Mtuhumiwa wa kesi ya matumizi mabaya ya fedha kwenye ujenzi wa jengo pacha la Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba akiwa kwenye chumba cha Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam,akisubiri kusikiliza rufaa yake mahakamani hapo jana. Picha na Michael Matemanga

Wednesday, August 25, 2010

GARI LA KUBEBA WAGONJWA LIKIWA KWENYE KAMPENI ZA CCM


Gari la kubeba wagonjwa la hospitali ya Rufaa ya Bugando likiwa kwenye msafara wa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete.

NDOA YA MCHEZA GOLFU MAARUFU DUNIANI YAVUNJIKA SASA


Sasa ni rasmi kwamba mcheza golfu maarufu duniani,Tiger Woods ametalikiana na mke wake, Elin Nordegren baada ya Woods kukiri kwamba alikuwa na mwanamke mwingine. Nordegren and Woods walioana Oktoba 5, mwaka 2004, huko Barbados na wana mtoto wa kike wa miaka mitatu na mwingine wa kiume wa miezi 18. Mpaka sasa haijafahamika Nordegren atapewa shilingi ngapi baada ya kutalikiana, lakini wadadisi wa mambo wanasema Nordegren atapata mamilioni ya dola za Kimarekani.

Tuesday, August 24, 2010

WAGOMBEA WA CUF WAFARIKI ZANZIBAR



Wagombea wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) wamefariki dunia jana visiwani Zanzibar katika matukio tofauti.Waliofariki dunia ni alikuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kojani (CUF), Omar Ali Jadi (55) Mkoa wa Kaskazini Pemba na Mwalimu Shani Hamada Shani ambaye ni mgombea wa udiwani wa chama hicho katika Jimbo la Kikwajuni. Jadi alikuwa akiugua ugonjwa wa kisukari na kwamba alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya figo. Shani alifariki dunia baada ya kugongwa na gari wakati akielekea kuchukua fomu katika Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC), eneo la Maisara.

MAFURIKO PAKISTANI YAENDELEA KUWATESA WATOTO

Mkazi wa Pakistani akiwa amembeba mtoto wake ambaye anaarisha kwenye hospitali ya Sukkur kutokana na athari za mafuriko. Rais wa Pakustani Asif Ali Zardari amesema leo kuwa nchi yake itachukua muda mrefu kuijenga nchi hiyo, kutokana na uharibifu uliosababishwa na marufiko. Dola 700 milioni za Marekani zinahitajika kwa ajili ya kuijenga nchi hiyo. Kutokana na mafuriko hayo, zaidi ya watu 1,500 wamepoteza maisha na wengine milioni 20 wameathirika. Picha na AFP/ Asif Hassan.

Saturday, August 21, 2010

KIKWETE AANGUKA WAKATI AKIHUTUBIA JANGWANI

Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), jana zimeingia dosari ikiwa ni siku ya kwanza katika uzinduzi wa kampeni zake katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam baada ya mgombea wake wa kiti cha urais, Jakaya Kikwete kuanguka jukwaani kutokana na kuishiwa nguvu.

Baada ya dakika 16 tangu alipoanza kuhutubia umati wa wanaCCM waliofurika katika viwanja hivyo, Kikwete alianza kuishiwa nguvu na kupepesuka, lakini walinzi wake walimdaka na kumpa msaada kwa kumdoa jukwaani.

Dakika 14 baadaye alirejea jukwaani huku akionyesha kuchoka na kuendelea na hotuba yake kwa dakika tano kabla ya kwenda kuketi meza kuu kwa dakika mbili na kuamua kuondoka katika viwanja hivyo.

Rais Kikwete aliwasili viwanja hivyo saa 7:45 mchana akifuatana na Mgombea Mwenza, Dk Mohamed Gharib Bilal na kupanda katika jukwaa kuu kuungana na viongozi kadhaa wa CCM na serikali akiwa na furaha.

WANACHAMA WA CCM WAKIWA WAMEFURIKA VIWANJA VYA JANGWANI

Friday, August 20, 2010

WATUHUMIWA WA UGAIDI WAKITOKA MAHAKAMANI


Watuhumiwa Hussein Hassan Agad (aliyevaa kanzu nyeusi) na Ismail na Ismail Abubakari wakitoka mahakamani Jumanne iliyopita mjini Kampala nchini Uganda. Watuhumiwa hao, wanadaiwa kuhusika katika mlipuko wa mabomu na kusababisha vifo vya watu 76 nchini humo wakati wakiangalia fainali za kombe la Dunia kati ya timu ya Taifa ya Hispania na Uholanzi. Mechi ya Fainali ilifanyika nchini Afrika Kusini mapema mwaka huu.

WAGOMBEA WA CHADEMA GEITA WAFANYIWA VITUKO


MWENYEKITI wa Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (Chasema) Wilaya ya Geita Mabura Kachoji amewashutumu wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wanawafanyia fujo wagombea udiwani wa chama chao.

Akizungumza na Mwananchi mwenyekiti huyo alibainisha kuwa wafuasi hao wamewafanyiwa fujo wagombea wao wawili na kwamba mgombea udiwani wa kata ya Rwamgasa Jimbo la Busanda Ntalima Masawe Paulo alichomewa Nyumba yake.
Kachoji alidai mbali na kuchomewa nyumba kwa mgombea huyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita Philimon Shelutete amekuwa akimkamata Mgombea huyo na kumfuga kwa madai ya kukwamisha shughuli za kimaendeleo.

Alieleza Paulo ametiwa ndani kwa amri ya mkuu huyo wa Wilaya mara tatu na kusababisha ashindwe kufuatilia shughuli za maendelo ya kata yake ambayo anagombea.

“Mimi sidhani kama kuna mtu anaweza kukwamisha shughuli za maendeleo hususani katika eneo ambalo anaishi na wakati huo huo, wananchi wa sehemu hiyo wakiwa wanamunga mkono awe kiongozi wao,”alisema Kachoji.

Alisemja Paulo ni mgombea mwenye sifa ya kuwa kiongozi na anaweza kutetea masilahi ya wananchi na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Katika tukio lingine, mgombea wa Kata ya Nyamgusu alivamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana na kumjeruhi kichwani baada ya kumpiga na nondo.

Kitendo hicho, kimemuathiri mgombea huyo kisaikolojia na amejitoa katika kinyanganyiro na chama kililazimika kumsimamisha mgombea mwingine kupitia Chadema.

Katika hatua nyingine ambayo inaonekana kuwa CCM imedhamiria kuwangoa wapinzani ni kitendo cha baadhi ya maofisa watendaji kufunga ofisi zao mara kwa mara pindi wanapogundua kuwa wagombea wa Chadema wanaenda katika ofisi zao kupata huduma.

Alisema matukio hayo yamekuwa ya kawaida kwa maofisa hao na mtendaji wa Kata ya Katoma alifanya kitendo hicho makusudi cha kutoka nje ya ofisi ili kumkwamisha mgombea wa Chadema wakati alipokuwa akirudisha fomu.

Alisema kutokana na hali hiyo, walifanya kazi ya ziada ya kumtafuta kwa njia ya simu ili waweze kupata huduma, lakini mtendaji huyo aliweka vikwazo vingi kama vile hana usafiri wa kumpeleka ofisini

“Kwa kuwa sisi tulikuwa na shida ilibidi tumfuate na usafiri wa pikipiki tuliokuwa nao,na tulipofika aligoma kupanda pikipiki hiyo kwa madai pikipiki ilikuwa na bendera ya Chadema. Lakini tulipomtishia kuwa tutapeleka malalamiko kwa Mkurugenzi wa Manispaa alikubali kupanda pikipiki,”alisema Kachoji.

Kachoji ilibidi atoe taarifa kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Geita Mpangalakela Katala na mkurugenzi huyo aliahidi kufuatilia malalamiko hayo. Habari hii, imeandikwa na Sheilla Sezzy,Geita

BALOZI WA UHOLANZI AKIZINDUA SHULE YA SEKONDARI LUSHOTO


Balozi wa Uholanzi nchini, Dr Ad Koekkoek akikata utepe wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari Prince Claus wilayani Lushoto alipoitembelea juzi. Shule hiyo imepewa jina hilo, ikiwa ni kumbukumbu ya marehemu mume wa Malkia wa Uholanzi, Beatrix Benhard ambaye masomo yake ya awali akiwa mdogo alianzia wilayani. Picha na Burhani Yakub.

FM ACADEMIA KUZINDUA ALBUM MPYA YA VUTA NIKUVUTE

Rais wa Bendi ya FM Academia, Nyoshi El- Saadat (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (pichani hawapo) kuhusu uzinduzi wa album yao ya sita ijulikanayo vuta nikuvute. Uzinduzi huo, utafanyika siku ya Idd Mosi katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. Kushoto ni Meneja wa Bendi hiyo, Mujib Khamis na Ofisa Habari wa Idara ya Habari Zahra Majid. Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es Salaam

WANANCHI MAMBO SAFIIIIIIIIIIIII, TUTASHINDAAAAA


Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete akiwahutumbia wanachama na wapenzi wa chama hicho kwenye ofisi ndogo za CCM zilizopo Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam jana baada ya kurejesha fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Picha na Edwin Mjwahuzi na Emmanuel Herman.

PROFESA LIPUMBA AKIREJESHA FOMU TUME YA UCHAGUZI



Profesa Ibrahim Lipumba (kushoto) ambaye ni mgombea urais wa CUF na mgombea mwenza, Juma Duni Haji wakisalimia wananchi wakati akiwasili Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam ili kurudisha fomu. Picha na Edwin Mjwahuzi.

Thursday, August 19, 2010

AFUNGWA BAADA YA KUKUTWA AKIUZA ALBINO SH 400 MILIONI


Raia wa Kenya Nathan Mutei (kushoto) jana amefungwa miaka tisa gerezani au kulipa faini ya Sh 80 milioni baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha albino kutoka Kenya kwa lengo la kumuuza Sh 400 milioni. Mtuhumiwa aliondoka Kitale nchini Kenya Agosti 12, mwaka huu na kuingia Tanzania kupitia mpaka wa Isibania kwa ajili ya kumuuza.

Mutei alipofika Tanzania alionana na mganga wa jadi na baadaye taarifa zilitolewa kwa maofisa wa jeshi la polisi kwamba kuna jamaa anauza albino akiwa hai. Kutokana na taarifa hizo, mtuhumiwa alikamatwa na jeshi hilo na baadaye kushtakiwa na kupatikana na hatia.

Mutei alihukumiwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mwanza, Angelous Rumisha baada ya kukiri makosa yake katika mahakama hiyo.

Katika kosa la kwanza, Mutei alidaiwa kumsafirisha binadamu kinyume na sheria namba 6 ya mwaka 2008 ya makosa ya kusafirisha binadamu.

Kosa la pili, mtuhumiwa anadaiwa kumteka mtu na kutaka kumuua na kuuza viungo vyake kinyume na kanuni za makosa ya adhabu namba 248 kifungu cha 16. Picha na Frederick Katulanda.

MAFURIKO PAKSTAN YAUA ZAIDI YA WA 1,000 MPAKA SASA

Mafuriko yaliotokea Kaskazini- Magharibi nchini Pakstan, yanakadiriwa kusababisha watu karibu 1,100 kupoteza maisha na wengine milioni moja wameathirika. Kutokana na hali hiyo, wakoaji na Mashirika ya Kimataifa ambayo yanatoa misaada yamekuwa yakiangaika kuokoa maisha ya watu. Umoja wa Mataifa (UN) umesema kuwa watoto wako hatarini kupata magonjwa ya kuambukiza. Marekani imetangaza kutoa msaada wenye thamani ya dola 10 milioni ili kuwasaidia watu walioathirika.  Picha na AFP
Picture by AFP
Picture by AFP

Wednesday, August 18, 2010

MASHABIKI WA YANGA LEO WAKISHANGILIA SIMBA KUFUNGWA MABAO 3-1 KATIKA UWANJA WA TAIFA

KOCHA WA YANGA KOSTADIN PAPIC 'CLINTON' AKIFURAHIA KUIFUNGA SIMBA MAGOLI 3-1

WAFANYAKAZI AFRIKA KUSINI WAANZA MGOMO KUPINGA NYONGEZA YA MSHAHARA

Wafanyakazi nchini Afrika Kusini leo wameanza mgomo rasmi kupinga nyongeza ya asilimia 7 ya mshahara walioongezewa na Serikali nchini humo. Vyama vya wafanyakazi vilivyo chini ya muungano wa Cosatu walipendekeza wafanyakazi waongezewe mshahara kwa asilimia 8.6, lakini serikali imeonekana kutoafiki mapendekezo ya chama hicho.

RAIS KIKWETE AKIZINDUA MNARA WA MASHUJAA WA MAJIMAJI

Rais Jakaya Kikwete akifungua rasmi mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa waliopigana vita vya Majimaji uliojengwa katika Kijiji cha Nandete, Kata ya Kipatimu wilayani Kilwa. Eneo hilo ni mahali ambako vita hivyo vilipangwa na kuanza.Picha na Freddy Maro.

Tuesday, August 17, 2010

MISS TANZANIA WAANZA KAMBI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania leo watasaini mikataba kati yao na waandaaji pamoja na kupewa semina maalumu na kamati ya mashindano hayo. Mbali na hayo, washiriki 31 kutoka kanda mbalimbali nchini jana walianza kambi kwenye hoteli ya Giraffe nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Monday, August 16, 2010

NDEGE YAKATIKA VIPANDE VITATU, ABIRIA WOTE WATOKA SALAMA


Abiria wote 125 na wafanyakazi sita waliokuwa wamepanda katika ndege Boeing 737 wametoka hai katika ndege hiyo leo baada ya kukatika vipande vitatu wakati ikijaribu kutua katika Kisiwa cha Kolombia. Gavana wa mji wa Bogota amesema ni maajabu watu wote kupona na mtu mmoja tu kufariki dunia katika ajali hiyo.

“Ilikuwa ni maajabu na hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu, ni mtu mmoja tu amepoteza maisha,” alisema Ofisa wa Jeshi la Anga nchini Kolombia, Pedro Gallardo (68). Kutokana na ajali hiyo, watu 119 wanatibiwa katika hospitali moja nchini humo na wengine watano ni mahututi katika hospitali hiyo.

KUMEKUCHA MAALIM SEIF ACHUKUA FOMU YA URAIS



Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Khatibu Mwinyichande akimkabidhi fomu za kugombea urais wa Zanzibar, Katibu Mkuu wa Civic United Front (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad (kushoto) kwenye ofisi za tume hiyo,Zanzibar jana. Picha na Emanuel Herman.

Friday, August 13, 2010

MNYIKA ACHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE UBUNGO



Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa Chadema, John Mnyika (kushoto) leo amechukua fomu za kugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo. Amesema katika uchaguzi ujao, amejipanga vizuri na atahakikisha anatafuta kura na kuzilinda ili zisiibwe kama Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005. Picha na Emanuel Herman

CHATU ALIYEPOTEA HUYU HAPA


Wananchi wakiwa wamembeba nyoka aina ya chatu aliyepotea katika eneo la Keko Keko Jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita na kusababisha hofu kwa wakazi wa eneo hilo, amepatikana jana ndani ya Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Da es Salaam.

Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Wizara hiyo, Erasmus Tarimo alisema nyoka huyo alipatikana leo saa 4:00 asubuhi ndani ya ofisi hizo baada ya juhudi za timu ya watu wanane kutoka katika kampuni mbalimbali zinazojishughulisha na uwindaji na ufugaji wa viumbe hai pamoja na askari 18 wa wanyamapori.

Baada ya kupatikana kwa nyoka huyo, hivi sasa wakazi wa Keko watalala na kuendelea na shughuli zao za kila siku bila hofu yoyote ya kuumwa na nyoka huyo. Picha na Silvan Kiwale.

Wacheza ngoma ya asili wakionyesha staili mbalimbali za kucheza kwenye sherehe ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa, William Lukuvi kufungua jengo jipya la uzazi na upasuaji katika Zahanati ya Roundtable iliyopo Mbagala jijini Dar es Salaam.

LUKUVI KATIKA MOJA YA KAZI ZAKE DAR ES SALAAM

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi akitoa pongezi kwa watengenezaji wa meza ya maabara yakuhamishika pamoja na kuizindua Shule ya Sekondari ya Mbagala Kuu jijini Da es Salaam. Meza hiyo, ina thamani ya shilingi 5 milioni na imenunuliwa na Manispaa ya Temeke ili kuwasaidia wanafunzi shuleni hapo kufanya mazoezi ya vitendo.

Thursday, August 12, 2010

Picha zote na Felix Mwagara, Salhim Shao na Edwin Mjwahuzi

NAPE HUYOOO AIBUKIA CHADEMA

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Nauye jana alienda kwenye Mkutano Mkuu wa Chadema na bila kuchelewa wajumbe wa mkutano huo, walikuwa wakijaribu kumvika tagi yenye picha ya mgombea wa urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa. Awali ilielezwa kuwa Nape alikuwa anataka kujiunga na Chadema baada ya kuangushwa kwenye kura za maoni katika Jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam. Lakini jana Nape alisema ni mwanachama wa CCM na ataendelea kubaki CCM.

SAMUEL SITTA NA ROSTAM AZIZI WAKITETA JAMBO


Viongozi hawa; Spika wa Bunge, Samuel Sitta akiteta na Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi kwenye Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi mjini Dodoma jana.

WAZIRI WA ZAMANI AFIKISHWA MAHAKAMANI


Waziri wa mkongwe wa serikali ya awamu ya kwanza hadi ya nne na aliyekuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini, Joseph Mungai amefikishwa jana katika Mahakama ya Mkoa wa Iringa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma za kutoa rushwa wakati wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kesi yake iko kwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa, Mary Senape na kwamba anatuhumiwa kufanya kosa hilo Julai 8, mwaka huu katika Kata ya Ihalimba.

AKATWA KWA PANGA KWA KUTOJUA KUPIKA CHAKULA KITAMU

Mkazi wa Kijiji cha Itununu wilayani Serengeti, Juliana Mark (20) akiwa amelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo baada kukatwa na panga kichwani, mkononi na mguuni kwa kuwa hajui kupika chakula kizuri.

WANACHAMA CCM WACHARUKA KURA ZA MAONI


Wanachama wa CCM jijini Dar es Salaam wakilalamika kwa Katibu Uenezi na Siasa Mkoa wa Dar es Salaam wa chama hicho, Juma Simba kuwa wagombea wao waliotangazwa washindi katika kura za maoni wameenguliwa.
Picha zote na Michael Jamson, Tumaini Msowoya, Anthony Mayunga na Edwin Mjwahuzi.

HII NDIO BONGO DAR ES SALAAM

Wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) wakiwa wamepanga bidhaa chini katika barabara ya Uhuru sehemu ya waenda kwa miguu eneo la Karume jijini Dar es Salaam.

Friday, August 6, 2010

MKE WA OBAMA 'AKITANUA' HISPANIA


Mke wa rais wa Marekani, Michelle Obama (mwenye miwani) akiwa nchini Hispania jana kwa ajili ya kutembelea mji wa kihistoria wa Marbella. Katika ziara hiyo, Michelle ameongozana na mtoto wake Sasha, wanaoonekana pembeni yake walinzi na mafariki wa familia ya rais Obama. Jamaii imekuwa ikilalamikia zaidi gharama anazotumia Michelle katika ziara zake za mapumziko.

WANAFUNZI 18 WAFA MAJI ZIWANI

KATIKA Mkoa wa Mwanza wanafunzi 18 wa Shule ya Msingi ya Chekechea ya Halukunbi wamefariki dunia baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kuzama kwenye Ziwa Victoria.

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza,Simon Sirro alisema ajali hiyo, ilitokea jana saa 1:45 asubuhi wakati wanafunzi wanaokadiriwa kuwa 37 walipokuwa wakisafiri kutoka Kisiwa cha Chitambele kwa ajili ya kwenda Kijiji cha Hulukumbi katika Wilaya ya Sengerema.

DK SLAA: WAFANYAKAZI NCHINI NIPIGIENI KURA ZENU 350,000


CHAMA cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema), kinaonekana kuwa na ushawishi mkubwa kwa wananchi na sasa kimewataka Watanzania, wakiwemo wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wafanyakazi 350,000 kumpigia kura mgombea urais wa Chadema katika uchaguzi mkuu ujao.


Mapema mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wazee wa Dar es Salaam baada ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA)kutangaza mgomo nchi mzima kuanzia Mei 15, mwaka huu, alisema hataki kura 350,000 za wafanyakazi hao, kwani ana uhakika wa kushinda nafasi ya urais oktoba. Kwa mujibu wa Dk Willibrod Slaa, Rais Kikwete alisema hata kama wafanyakazi wote wasipomchagua hana haja na kura zao.

Hayo yalisemwa mkoani Mtwara katika mkutano wa hadhara jana uliofanyika viwanja vya mashujaa mjini hapa wakati Dk Slaa akiomba kudhaminiwa na wananchi ili kugombea nafasi ya urais.

Thursday, August 5, 2010

FAHARI YA TANZANIA

Hii ni fahari ya Tanzania. Watanzania tujivunie maliasili zetu. Kiboko akiwa katika hifadhi ya SERENGETI.

Wednesday, August 4, 2010

WAFUASI WA DK SLAA NA WA RAIS KIKWETE WAZOMEANA


WAFUASI wa mgombea urais kwa chama cha Chadema Dk Willibrod Slaa na wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokuwa wakisubiri kumdhamini Rais Jakaya Kikwete nusura wazue mtafaruku baada kupishana na kuzomeana.


Tukio hilo lilitokea saa 6:30 mchana wakati wafuasi wa Chadema walipokuwa wametoka kumpokea Dk Slaa uwanja wa ndege wakapishana katika eneo la ofisi za CCM mkoa walipokuwapo wale wa CCM wakisubiri kumdhamini Rais Kikwete katika harakati zake za urais.

MREMA ASHANGILIA KIMARO KUANGUSHWA VUNJO


MWENYEKITI wa Tanzania Labour Party (TLP), Agustino Mrema, jana alitembea zaidi ya kilometa 10 kwa miguu kuudhihirishia umma kuwa ana afya nzuri wakati akienda kuchukua fomu za kugombea Ubunge katika Jimbo la Vunjo.


Mrema akiwa na mgombea urais kupitia tiketi ya chama hicho,Mutamwega Mganywa, walitembea kwa miguu kutokea Kijiji cha Chekereni hadi mji mdogo wa Himo,huku akisindikizwa na mamia ya wanachama.

Wanachama hao wakiwa wamevalia fulana za njano zenye nembo ya TLP na maneno "Vunjo hatudanganyiki", walikuwa wakishangilia na vijana waliokuwa wakiendesha pikipiki zaidi ya 40, wakifanya vituko mbalimbali kama ishara ya kushangilia.

Mrema aliwapongeza wanachama wa CCM wa Jimbo la Vunjo kwa kuamuangusha Mbunge aliyemaliza muda wake, Aloyce Kimaro katika kura za maoni.

"Wana-CCM Vunjo ni watu wazuri sana hongereni kwani mlichokifanya ni jambo zuri la kumuondoa Kimaro. Kimaro ana fedha nyingi hivyo, angenisumbua sana,"alitamba Mrema.

Katika mchakato wa kura za maoni, Wakili na Mwanasheria wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii(NSSF), Chrispin Meela aliongoza kwa kupata kura 7,732 dhidi ya Kimaro aliyepata kura 3,207 na hivyo kushindwa kutetea kiti chake.

UMATI WA WANAFUNZI WAKIFANYA MTIHANI ILI WAAJIRIWE

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakifanya mtihani jana katika chuo hicho, ulioandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa ajili ya kuwaajiri katika kampuni hiyo. Umati wa wanafunzi hao, unaonyesha jinsi tatizo la ajira lilivyokubwa nchini. Pengine wanaohitajika kuajiriwa ni watu sita tu kati ya watu 200 waliofanya mtihani.

WANAFUNZI 80 WANUSURIKA KUTEKETEA KWA MOTO

WANAFUNZI 80 waliokuwa wamelala katika bweni la Nyerere Shule ya Sekondari Rugambwa Manispaa ya Bukoba wamenusurika kufariki dunia baada ya bweni hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana. Tukio hilo, lilitokea saa 2:30 usiku wakati wanafunzi hao wakiwa wanasoma madarasani.Katika tukio hilo, vifaa vyote vya wanafunzi viliteteketea kwa moto.

Mwandishi wa Mwananchi ambaye alikuwa eneo la tukio alishuhudia zaidi ya wanafunzi 15 wakizimia na kupoteza fahamu na baadaye kukimbizwa katika hospitali ya mkoa Kagera kwa matibabu zaidi. Mazingira ya shule hiyo yalitawaliwa na vilio vya wananchi na wanafunzi katika giza nene na kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kagera Henry Salewi alikuwa miongoni mwa viongozi walioshiriki kuimarisha usalama katika eneo hilo.

Mkuu wa sekondari hiyo ya wasichana Asha Mbanga alipoulizwa kwa njia ya simu alisema hana taarifa kuhusu tukio hilo kwani alikuwa safarini kutoka jijini Mwanza.

ALAWITIWA BAADA YA KUNYWA POMBE NYINGI

JESHI la polisi linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Kalungwa Tarafa ya Mkuyuni Wilaya ya Morogoro kwa tuhuma za kumlawiti mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 31.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Thobias Andengenye alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 1 mwaka huu,saa 2:30 katika kijiji hicho baada ya mtu huyo kupoteza fahamu baada ya kunywa pombe kupita kiasi na kulewa chakari.

Alimtaja mtuhumiwa wa tukio hilo kuwa ni Bahati Said na kwamba mtu huyo alilawitiwa wakati akitokea kilabuni baada ya kuzidiwa na pombe na kusababisha kuanguka na kulala vichakani na mtuhumiwa huyo wakati akipita katika eneo hilo, alimkuta na kumlawiti. Mtu huyo ametibiwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro na kwamba uchunguzi zaidi wa polisi unaendelea kuhusiana na tukio hilo .

Mtikila akwepa kifungo gerezani



MWENYEKITI wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila amekubali kulipa deni alilokuwa anadaiwa na Paskazia Matete la Sh 9.8 milioni na kuachiwa huru.

Kama Mchungaji huyo ambaye ametangaza kugombea urais kupitia chama chama cha DP asingelipa deni hilo, angetumikia kifungu cha miezi sita gerezani na tayari juzi alianza kuonja joto la jiwe baada ya kulala mahabusu ya kituo cha polisi cha Msimbazi kwa kushindwa kulipa deni hilo.

Mtikila alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela bila ya kuwepo mahakamani Julai 29 baada ya mahakama kukubali ombi la mdai huyo. Hakimu Joyce Minde alitoa hukumu hiyo kwa sharti kwamba ianze kutekelezwa baada ya Paskazia kulipa Sh600,000 kwa ajili ya gharama za kumhudumia mchungaji huyo wakati atakapokuwa kifungoni.Mwanamke huyo alilipa fedha hizo na ndipo hukumu hiyo ilipoanza kutekelezwa.

Tuesday, August 3, 2010

Utata wa Malecela na Lusinde watatuliwa


Hatimaye CCM wilayani Chamwino jana ilimaliza utata kwenye matokeo ya kura za maoni katika jimbo la Mtera ilipotangaza kuwa mwanasiasa mkongwe, John Malecela ameangushwa baada ya habari kusambaa kwa kasi kubwa kuwa Livinstone Lusinde hakuwa ameshinda.
Habari za ushindi wa Lusinde zilifunikwa na taarifa iliyosambaa kwa kasi jana kuwa mshindi wa kura za maoni kwenye jimbo hilo bado hajatangazwa rasmi na kwamba Malecela ndiye aliyekuwa akiongoza kwa kupata kura 5,652 dhidi ya 5,407 za Lusinde licha ya katibu wa CCM mkoani Dodoma kumtangaza kijana huyo kuwa ndiye mshindi.

Lakini jana, mkurugenzi wa uchaguzi wa CCM wilayani Chamwino ambaye pia ni katibu wa chama hicho kwenye wilaya hiyo, Edson Lihweuli aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kumtangaza Lusinde kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM kwenye uchaguzi mkuu ujao na hivyo kuthibitisha habari za kuanguka kwa Malecela, maarufu kama "tingatinga".