Monday, August 16, 2010

NDEGE YAKATIKA VIPANDE VITATU, ABIRIA WOTE WATOKA SALAMA


Abiria wote 125 na wafanyakazi sita waliokuwa wamepanda katika ndege Boeing 737 wametoka hai katika ndege hiyo leo baada ya kukatika vipande vitatu wakati ikijaribu kutua katika Kisiwa cha Kolombia. Gavana wa mji wa Bogota amesema ni maajabu watu wote kupona na mtu mmoja tu kufariki dunia katika ajali hiyo.

“Ilikuwa ni maajabu na hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu, ni mtu mmoja tu amepoteza maisha,” alisema Ofisa wa Jeshi la Anga nchini Kolombia, Pedro Gallardo (68). Kutokana na ajali hiyo, watu 119 wanatibiwa katika hospitali moja nchini humo na wengine watano ni mahututi katika hospitali hiyo.

No comments:

Post a Comment