Wednesday, August 4, 2010

WAFUASI WA DK SLAA NA WA RAIS KIKWETE WAZOMEANA


WAFUASI wa mgombea urais kwa chama cha Chadema Dk Willibrod Slaa na wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokuwa wakisubiri kumdhamini Rais Jakaya Kikwete nusura wazue mtafaruku baada kupishana na kuzomeana.


Tukio hilo lilitokea saa 6:30 mchana wakati wafuasi wa Chadema walipokuwa wametoka kumpokea Dk Slaa uwanja wa ndege wakapishana katika eneo la ofisi za CCM mkoa walipokuwapo wale wa CCM wakisubiri kumdhamini Rais Kikwete katika harakati zake za urais.

No comments:

Post a Comment