Friday, August 13, 2010

CHATU ALIYEPOTEA HUYU HAPA


Wananchi wakiwa wamembeba nyoka aina ya chatu aliyepotea katika eneo la Keko Keko Jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita na kusababisha hofu kwa wakazi wa eneo hilo, amepatikana jana ndani ya Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Da es Salaam.

Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Wizara hiyo, Erasmus Tarimo alisema nyoka huyo alipatikana leo saa 4:00 asubuhi ndani ya ofisi hizo baada ya juhudi za timu ya watu wanane kutoka katika kampuni mbalimbali zinazojishughulisha na uwindaji na ufugaji wa viumbe hai pamoja na askari 18 wa wanyamapori.

Baada ya kupatikana kwa nyoka huyo, hivi sasa wakazi wa Keko watalala na kuendelea na shughuli zao za kila siku bila hofu yoyote ya kuumwa na nyoka huyo. Picha na Silvan Kiwale.

1 comment: