Friday, August 6, 2010

DK SLAA: WAFANYAKAZI NCHINI NIPIGIENI KURA ZENU 350,000


CHAMA cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema), kinaonekana kuwa na ushawishi mkubwa kwa wananchi na sasa kimewataka Watanzania, wakiwemo wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wafanyakazi 350,000 kumpigia kura mgombea urais wa Chadema katika uchaguzi mkuu ujao.


Mapema mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wazee wa Dar es Salaam baada ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA)kutangaza mgomo nchi mzima kuanzia Mei 15, mwaka huu, alisema hataki kura 350,000 za wafanyakazi hao, kwani ana uhakika wa kushinda nafasi ya urais oktoba. Kwa mujibu wa Dk Willibrod Slaa, Rais Kikwete alisema hata kama wafanyakazi wote wasipomchagua hana haja na kura zao.

Hayo yalisemwa mkoani Mtwara katika mkutano wa hadhara jana uliofanyika viwanja vya mashujaa mjini hapa wakati Dk Slaa akiomba kudhaminiwa na wananchi ili kugombea nafasi ya urais.

No comments:

Post a Comment