Wednesday, August 4, 2010

ALAWITIWA BAADA YA KUNYWA POMBE NYINGI

JESHI la polisi linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Kalungwa Tarafa ya Mkuyuni Wilaya ya Morogoro kwa tuhuma za kumlawiti mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 31.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Thobias Andengenye alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 1 mwaka huu,saa 2:30 katika kijiji hicho baada ya mtu huyo kupoteza fahamu baada ya kunywa pombe kupita kiasi na kulewa chakari.

Alimtaja mtuhumiwa wa tukio hilo kuwa ni Bahati Said na kwamba mtu huyo alilawitiwa wakati akitokea kilabuni baada ya kuzidiwa na pombe na kusababisha kuanguka na kulala vichakani na mtuhumiwa huyo wakati akipita katika eneo hilo, alimkuta na kumlawiti. Mtu huyo ametibiwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro na kwamba uchunguzi zaidi wa polisi unaendelea kuhusiana na tukio hilo .

1 comment: