Friday, August 6, 2010

WANAFUNZI 18 WAFA MAJI ZIWANI

KATIKA Mkoa wa Mwanza wanafunzi 18 wa Shule ya Msingi ya Chekechea ya Halukunbi wamefariki dunia baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kuzama kwenye Ziwa Victoria.

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza,Simon Sirro alisema ajali hiyo, ilitokea jana saa 1:45 asubuhi wakati wanafunzi wanaokadiriwa kuwa 37 walipokuwa wakisafiri kutoka Kisiwa cha Chitambele kwa ajili ya kwenda Kijiji cha Hulukumbi katika Wilaya ya Sengerema.

No comments:

Post a Comment